EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, August 13, 2014

Polisi Moro: Hatushuki daraja Ng'o


NA SHARIFA MMASI
KOCHA mkuu wa maafande wa Polisi Morogoro Mohamed Richard Adof,  amesema kikosi chake kinaendelea na mazoezi kabambe, hawatashuka daraja tena
Kocha huyo alisema kikosi chake kinaendelea na mzoezi makali ambayo yataleta mafanikio katika timu ikiwa ni pamoja na  kuondoa sura mbaya ya timu hiyo ya kupanda na kushuka daraja kila msimu.
 
"Kikosi changu kinaendelea na mazoezi makali ya kuhakikisha hakuna timu itakayotufunga kutokana na mbinu nilizowapa wachezaji wakati wa mazoezi na wanapocheza mechi mbali mbali za kirafiki.," alisema Adof.
Adol alisema kila timu inafanya maandalizi ya nguvu kwa ajili ya kuleta ushindani kwenye Ligi, kwa kutambua hilo wanajitahidi kujipanga vizuri ili kuja kukabilia na changamoto za Ligi hiyo.
Timu ya Polisi ilishuka daraja msimu wa mwaka 2012/13 pamoja na timu za African Lyon na Toto African ya Mwanza kabla ya kufanikiwa kupanda tena msimu huu.
 

No comments:

Post a Comment