EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, January 8, 2014

YANGA YAMWAGA MAMILIONI KOMBE LA MAPINDUZI


Pamoja na kushindwa kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi kutokana na kutokuwa na benchi la ufundi, Yanga imeonyesha heshima kubwa kwa michuano hiyo inayoendelea mjini Zanzibar.


Taarifa kutoka ndani ya Yanga zinaeleza, uongozi wa klabu hiyo umepanga kumwaga kiasi cha Sh milioni 10 ili kuisaidia michuano hiyo.
“Kweli Yanga ilishindwa kushiriki michuano hiyo kutokana na kutokuwa na benchi la ufundi. Lakini heshima bado iko juu na tunaiheshimu sana.

“Uongozi umeamua kuchangia gharama za kuendesha michuano hiyo kwa kuwa tunajua umuhimu na heshima ya Yanga visiwani Zanzibar.
“Pamoja na hivyo, siku tukiwa na nafasi, basi timu itakwenda Zanzibar kucheza na kombaini ya huko kwa ajili ya kuonyesha kuwa tunathamini,” kilieleza chanzo.
Uongozi wa juu wa Yanga ndiyo uliofikia uamuzi huo ili kuonyesha kuwa haukuwa na nia ya kuidharau michuano hiyo.
Wakati ulipofika kwenda kwenye michuano hiyo, Yanga ndiyo ilikuwa imetimua benchi lake lote la ufundi chini ya Kocha Ernie Brandts, raia wa Uholanzi.
Sasa Yanga bado inahaha kusaka kocha mkuu, huku msaidizi wake akiwa ni Charles Boniface Mkwasa ambaye anasaidia na kocha wa makipa, Juma Pondamali.
Yanga inaondoka kesho alfajiri kwenda nchini Uturuki ambako itaweka kambi katika mji wa Antalya.

Hii ni mara ya pili Yanga kuweka kambi katika mji huo wa kitalii nchini Uturuki.
SOURCE:SALEHE JEMBE

No comments:

Post a Comment