Kiungo wa timu ya Yanga, Athuman Idd ‘Chuj
KIUNGO mkabaji wa zamani wa Yanga ambaye sasa
anacheza soka la kulipwa Nepal nchini India, Godfrey Bonny amemuita
kiungo wa timu hiyo, Athuman Idd ‘Chuji’ nchini humo.
Kauli hiyo ameitoa baada ya kupata taarifa ya
kusimamishwa kiungo huyo hivi karibuni kwa kile kinachodaiwa ni utovu wa
nidhamu aliounyesha kwenye timu hiyo katika mechi ya Nani Mtani Jembe
na kumalizika kwa Yanga kufungwa mabao 3-1 dhidi ya Simba.
Akizungumza na Mwanaspoti, Bonny alisema anaamini
kiungo huyo ana uwezo mkubwa wa kucheza soka la kulipwa kama alivyokuwa
yeye ndani ya uwanja.
Bonny alisema Chuji asikatishwe tamaa kwa hali
hiyo iliyotokea na badala yake aendelee kufanya mazoezi kwa bidii ili
kiwango chake kisishuke.
Aliongeza kuwa anashangazwa na aina ya soka la
Tanzania ambalo wenyewe wanataka mchezaji kila wakati awe kwenye kiwango
cha juu bila kufahamu mwili wa binadamu unachoka ukitumika sana kama
iliyotokea kwa Chuji.
“Nimepata taarifa za Chuji kusimamishwa na Yanga,
ninashangazwa na mfumo wa uendeshaji wa viongozi wa soka ambao timu
ikifungwa tu, basi wanatafuta mchawi kwa kusimamisha wachezaji kwa madai
ya kuchukua rushwa kitu ambacho siyo sahihi.
“Nimtoe hofu Chuji kwa kumwambia aendelee kufanya
mazoezi kwa bidii ili kiwango chake kisishuke na kama akifukuzwa kabisa
basi nitamuita huku Nepal kuja kucheza soka la kulipwa nafasi zimejaa
tele.
“Ninaamini hataniangusha kutokana na na uwezo wake
ndani ya uwanja anacheza soka la akili na nguvu nyingi ni kati ya
wachezaji ninaowakubali nchini,” alisema Bonny anayecheza katika klabu
ya Saraswot Youth Club.SOURCE: MWANASPORT
No comments:
Post a Comment