Chama cha mapinduzi ( CCM) manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro kimeendelea
kusisitiza kuwa chama cha demokrasia na maendeleo, CHADEMA hakitaweza kushika
dola kutokana na mfumo wake wa utawala kuwa mbovu....
Kauli
hiyo ilitolewa jana na mwenyekiti wa CCM manispaa ya Moshi, Elizabeth Minde
wakati alipokuwa akimnada mgombea wa udiwani wa kata ya Kiboriloni kwa tiketi
ya chama hicho, Willy Adriano...
Mwenyekiti
huyo alisema migogoro inayoendelea ndani ya chama hicho ni ishara ya utawala
mbovu unaotokana na udikteta, udini na ukabila, hivyo chama hicho kupewa dola
ni kuhatarisha amani ya nchi hii ambayo imekuwa nembo ya taifa hili
kimataifa...
Alisema
CCM imejipanga vya kutosha kupata ushindi katika uchaguzi huo huku
akiwatahadharisha wanaoibeza CCM kuwa tayari kuingia aibu ufikapo februari 9
maka huu...
"Ili mwananchi aweze kupata maendeleo tunahitaji kupata kiongozi makini ambaye ataweza kuwaletea wananchi maendeleo, hivyo nawaomba wananchi wa kata ya Kiboriloni wamchague Willy Adriano, CCM ushindi unakuja"..Alisema Minde
Kwa
upande wake katibu mwenezi wa CCM mkoa, Michael Mwita, alisema kazi ya CCM ni
kuisimamia serikali katika kutekeleza shughuli za kimaendeleo kutokana na ilani
ya chama hicho.
"Asilimia
90 ya wakazi wa Kiboriloni wanakabiliwa na changamoto lukuki, huwezi kuwa na
mbunge ambaye ana maslahi yakwake.Kuna wapanda mlima wamekuwa wakinyanyasika na
malipo yao duni, lakini imekuwa ngumu kwa mbunge huyo kuwatetea vijana
hao" Alisema Mwita
Aliongeza
kuwa mbunge huyo tangu achaguliwe mwaka 2000 hakuna maendeleo yoyote
aliyowaletea wananchi wa Moshi pamoja na kutoa ahadi lukuki ikiwemo ahadi ya
kurudisha soko la Kiboriloni ambalo kwa sasa limehamishwa.
Alisema
mbunge huyo hana nia ya dhati ya kuwakomboa wananchi wake tofauti na anavyodai
katika majukwaa ya siasa na kuongeza kuwa mwaka 2010 aliwaahidi wamachinga kuwa
endapo watamchagua na kumpa halmashauri atahakikisha machinga hawanyanyaswi
huku akiahidi kuwajengea machinga complex, ahadi ambayo haijatekelezwa hadi
sasa.

No comments:
Post a Comment