Iran na mataifa yenye nguvu duniani, wameshindwa kufikia makubaliano hii leo
Jumapili, kuhusu mpango wa Nyuklia wa Iran, licha ya mazungumzo ya muda mrefu
mjini Geneva.
Hali hiyo imeondoa matarajio ya makubaliano yaliyotarajiwa kwa muda mrefu
katika msuguano huo wa muongo mmoja.
Hata hivyo
wanadiplomasia wamesema maendeleo makubwa yamefikiwa katika siku tatu za
majadiliano makali, na kwamba mazungumzo hayo yataanza tena mnamo Novemba 20.
Matumaini yaliongezeka baada ya
wanadiplomasia wa juu duniani kuwasili mjini Geneva, kujiunga na mazungumzo
hayo, lakini yalififia baada ya baada ya nyufa kuanza kuonekana miongoni mwa
mataifa yenye nguvu baada ya Ufaransa kuonesha wasiwasi.Makubaliano yanayotumainiwa yameonekana kama hatua ya mwanzo, kabla ya mazungumzo zaidi kuhusu makubaliano ya mwisho, na huenda yakaishuhudia Iran ikifungia juhudi zake za nyuklia kwa muda wa miezi sita, kama mbadala wa kuondokana na vikwazo ambavyo vimeharibu uchumi wake.
No comments:
Post a Comment