EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Sunday, November 10, 2013

SERIKALI YAZIKOROMEA ALMASHAURI NCHINI KUHUSU CHAKULA



Serikali imetoa wito kwa halmashauri nchini, zinazohusika katika mikoa itakayokabiliwa na njaa, kufuatilia kwa karibu utaratibu wa kupata chakula kinachotolewa kutoka maeneo yenye ziada, na kuhakikisha kuwa kinafika mapema kwenye maeneo yao, kabla ya wananchi wa maeneo hayo hawajaanza kulalamika.
 
Waziri mkuu wa Tanzania MH:Mizengo Pinda
Wito huo wa serikali umetolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakati akisoma hotuba ya kuahirisha Bunge la 10, katika Mkutano wa 13 mjini Dodoma, ambaye amesema halmashauri 61 zinatarajiwa kukumbwa na uhaba wa chakula. Ameitaja mikoa ya halmashauri zitakazokabiliwa na uhaba huo kuwa ni Manyara, Shinyanga, Simiyu, Arusha, Dodoma, Lindi, Tanga, Singida, Mara, Morogoro, Kilimanjaro, Mwanza, Pwani, Mtwara, Kigoma na Tabora.Waziri mkuu amesema serikali inaendelea na tathmini ya kina ya hali ya chakula na lishe katika halmashauri 61, kwa lengo la kubainisha idadi ya watu wenye uhaba wa chakula ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hilo Amewataka Wakala wa Taifa na Hifadhi ya Chakula, kujipanga vizuri kuhamisha chakula kutoka maeneo yenye ziada na kupeleka kwenye maeneo yenye hali tete ya uhaba wa chakula.

No comments:

Post a Comment