EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Saturday, October 12, 2013

MTWARA WAOMBWA KUWAKUMBATIA WAFADHILI KATIKA NYANJA YA ELIMU



WAZAZI na walezi mkoani Mtwara wamekumbushwa kutunza na kulinda matumizi bora ya miundombinu ya elimu inayotolewa na wafadhili kwa watoto wao, ili kuifanya iwe endelevu na kumsaidia mwanafunzi kujifunza na kuwa na ubora wa ufaulu. 
wazili wa nchi ofisi ya waziri mkuu tawala za mikoa na serikali za mitaa MH: AWA GHASIA
 Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe.Hawa Ghasia, wakati wa ugawaji wa msaada wa Taa za nguvu ya solar katika kata ya Dihimba, kwa wanafunzi wanaosoma katika shule nne za msingi kutoka katika kata hiyo.
Waziri huyo ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Mtwara Vijijini, amewahimiza wazazi na walezi hao kuwasimamia na kuhakikisha watoto hao wanazitumia taa hizo kwa lengo la kujisomea, kutokana na elimu kuchukua wigo mpana katika kujiletea maendeleo endelevu.
Msaada huo uliotolewa na Hotel ya Double Tree kutoka jijini Dar es salaam wenye jumla ya Taa za solar 200, umelenga kuwasaidia wanafunzi wanaosoma darasa la sita kwa ajili ya kujisomea wakati wakijiandaa kuingia darasa la saba, kwa lengo la kuongeza ubora katika kujisomea na kuongeza ufaulu.
WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MKOANI MTWARA
 Waziri Ghasia amesema kuwa msaada huo umezinufaisha shule nne za kata ya Dihimba, ambazo ni Dihimba yenyewe iliyopata taa 104, shule ya msingi Namanjele taa 39, Muungano taa 27 na Miuta taa 30.
Awali akizungumza katika makabidhianao hayo mkurugenzi wa mauzo wa Hoteli ya Double Tree Florenso Kirambata, amesema kuwa dhumuni hasa ni kuwelimisha wanafunzi chanzo kingine cha umeme kupitia taa hizo, ambazo zinaweza kutumika kwa masaa manne na kudumu kwa miaka kumi.                          

No comments:

Post a Comment