EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Tuesday, October 22, 2013

ADHABU YA VIBOKO YAWA KIKWAZO ELIMU TANZANIA



Walimu wametakiwa kupunguza adhabu za viboko kwa wanafunzi, na kuwapa adhabu nyingine mbadala kwani viboko peke yake sio suluhu la kumrekebisha mwanafunzi.


Akizungumza na mwandishi wa kituo hiki mapema hii leo ofisini kwake mkuu wa shule ya msingi ligula mwalimu tumaini mwangata amesema kuwa kumchapa mwanafunzi ni kumuondolea hadhi yake na kumfanya kuwa na nidhamu ya woga.Pia amesema kuwa kumpunguzia mwanafunzi adhabu ya viboko kunajenga mahusiano mazuri kati yake na mwalimu na kumfanya awe anasikiliza na kuelewa kile mwalimu anachomfundisha.Hata hivyo amewataka wazazi kusaidiana na walimu kwa kufuatilia maendeleo ya watoto wao pamoja na kulipa michango mbalimbali ya shule na kuhudhuria katika vikao mbalimbali vya shule vinavyolenga kujadili mwenendo wa watoto wao.

No comments:

Post a Comment