EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Tuesday, September 24, 2013

VIONGOZI wa Jumuiya ya wazazi wilayani Lushoto, mkoani Tanga, wameshauriwa kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wafanye juhudi kwasababu siasa za wakati huu zimejaa ushindani na kunahitajika utekelezaji wa sera zilizowekwa ili kuweza kukipatia Chama cha Mapinduzi (CCM) ushindi wa kishindo mwaka 2015.

a maktaba yetu.

Akizungumzia suala hilo, Mwenyekiti  wa  Wazazi  Mkoani  Tanga  Dkt Edmund Mndolwa, alisema hayo katika ziara ya  kuwashukuru kwa kumchagua kwa  kishindo katika  nafasi  hiyo ya  kuwa  mwenyekiti  wa Jumuiya hiyo na kutembelea wilaya zote 9 za Mkoa wa Tanga.
Alisema imekuwa ni jambo la kawaida kwa wenyeviti na Makatibu kufanya kazi kimazoea kwa kufanya kazi zisizo eleweka kwa kigezo cha kuwa Chama Cha Mapinduzi tayari ni chama kikubwa na kinapendwa na kuza hofu kwa mustakabali wa siasa za Tanzania.

Waziri Chizza aingilia kati mgogoro wa wakulima wa Chai wilayani Lushoto, mkoani Tanga



Na  Ray Said, Bumbuli
WAZIRI  wa  Chakula, Kilimo  na  Ushirika, Injinia Christopher  Chizza, amependekeza kuundwa kwa menejimenti ya muda katika kiwanda cha chai cha Mponde kama njia ya kusuluhisha mgogoro uliopo kati ya wakulima wa chai na mwekezaji wa kiwanda hicho, Kampuni ya Chai Lushoto.  
 Injinia Christopher  Chizza, katikati.
Akizungumza katika mkutano wa  hadhara  uliofanyika  katika  uwanja  wa  mazoezi katika kata ya Mponde, Chiza  pia aliahidi kushughulikia mgogoro uliopo kati ya wakulima hao wa chai na mwekezaji wa kiwanda cha chai cha Mponde, kilichopo Bumbuli, mkoani Tanga, ili kiendelee kutoa huduma bora.

 Alisema katika kumaliza mgogoro huo, atazungumza na Waziri Mkuu, Mizengo  Pinda kuhusu suala hilo ili kusaidia kupata ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro huo.
"Nitaishauri  serikali  kuchukua  kiwanda  hicho  na  baadaye   kuwakabidhi  wananchi  ambao  ndio  wamiliki  wa  kiwanda  hicho," alisema.

No comments:

Post a Comment