TAARIFA
KWA VYOMBO HABARI
YAH:SABABU
ZA KUUNGA MKONO UAMUZI WA MSAJILI WA VYAMA VYA MICHEZO NA VILABU KUKATAA
KUSAJILI MAREKEBISHO YA KATIBA YA TFF KUTOKANA UKIUKWAJI
WA UTARATIBU NA SHERIA ZA MAREKEBISHO YA KATIBA TFF 2013
Michael Wambura, pichani
Katiba ya TFF ya 2012 ilifutwa na msajIli wa vyama
vya michezo na vilabu kwa kuwa ilibadilishwa kinyume cha sheria(BMT) pamoja na Katiba ya TFF ibara ya 30 kwa kutumia njia ya waraka badala ya Mkutano
Mkuu, hivyo katiba halali kisheria
inayotambulika ni ile ya 2006 na mabadiliko yake . FIFA na Serekali kupitia wizara yenye dhamana
na michezo iliiagiza TFF iitishe Mkutano Mkuu ili ifanye mabadiliko
ya katiba stahiki kwa mujibu wa katiba
na kwa kufuata taratibu zilivyoainishwa kwenye katiba ya TFF. Nimelazimika kuendelea
kuiunga mkono Serikali kupitia msajili kwa maamuzi yake ya kukataa kusajili
mabadiliko ya katiba ya TFF kwa kuwa
TFF kwa makusudi imeendelea kuvunja katiba yake katika kufanya
mabadiliko.
January Makamba, Kagasheki waipiga tafu Habari Group kusaidia watoto yatima jijini Dar es Salaam
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
WANACHAMA wa Kikundi
cha Waandishi wa habari wanaojihusisha na ujasiriamali (Habari Group), wametoa
msaada wa vyakula na nguo wenye thamani ya sh. milioni moja kwa vituo viwili
vya kulelea watoto yatima kwa ajili ya sikukuu ya Idd El Fitri.
January Makamba, Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia
Msaada
huo uliofadhiliwa na wadau mbalimbali ulikabidhiwa juzi, na wanakikundi hao
ikiwa ni njia ya kuonyesha ushiriki wao katika masuala ya jamii.
Vituo
vilivyokabidhiwa msaada huo ni Kituo cha Kulelea watoto yatima cha
Tahfidhil-Qur-An Al-Hidaya kilichopo Buguruni na kituo cha Al Furqaan Islamic
kilichopo Chanika.
Mkuu wa Mkoa Singida atembelea banda la Wizara ya Uchukuzi, katika maonyesho ya wakulima mjini Dodoma
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Dkt. Parseko V. Kone, akimskiliza Afisa Huduma za Abiria wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), Bw. Peter Ngwale(wa pili kulia) wakati alipotembelea banda la Mamlaka hiyo leo mchana, katika maonesho ya Kilimo nanenane yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nzuguni,Dodoma.


No comments:
Post a Comment