EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, July 10, 2014

ORIGI WA KENYA ATUA LIVERPOOL KUPIGA MKATABA


Mbelgiji Divock Origi ametua kwenye makao makuu ya klabu ya Liverpool, leo kwa ajili ya kukamilisha masuala ya usajili.
Liverpool iko tayari kutoa kitita cha pauni milioni 30 kuwanasa Origi na winga wa Benfica, Lazar Markovic.
Taarifa zimesema wawili hao watakuwa na shughuli ya vipimo kesho na kama mambo yakienda sawa watamwaga wino kukipiga Anfield.
PICHA IKIMUONYESHA ORIGI ALIVYOTUA LEO NDANI YA LIVERPOOL

Imeelezwa Liverpool itatoa pauni milioni 19.8 kwa ajili ya uhamisho wa Markovic na pauni milioni 10 zitalipwa kwa Lille ya Ufaransa anayokipiga Origi.
Origi alionyesha uwezo mkubwa kwenye michuano ya Kombe la Dunia na timu yake iling’olewa na Argentina katika hatua ya robo fainali.

No comments:

Post a Comment