Mwenyekiti
wa Tancraft, Elihaika Mrema akizungumza na waandishi wa habari umuhimu
wa jumuiya kubwa za wafanyabiashara na pamoja na serikali kuwaunga mkono
wajasirimali wanawake nchini, Kushoto ni Esther Kasenga Msaidizi wa
Katibu, Kulia Mweka hazina wa Chama cha Tancraft, Bi.Louise Judicate na
Wapili kulia ni Katibu wa Tancraft, Bi. Vicky Shayo.
WAMILIKI Wote wa maeneo ya biashara nchini wameombwa
kutoa nafasi ya maeneo ya biashara kwa wajasirimali wanawake ili
kumkomboa mwanamke kutoka katika dimbwi la umaskini na utegemezi.
Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wajasirimali wanawake
jijini Dar es Salaam leo mchana, Mwenyekiti wa Tanzania Handcraft
Association (Tancraft), Elihaika Mrema amesema kuwa wanawake
wafanyabiashara wadogo wana matatizo na changamoto kadhaa mojawapo ni
maeneo ya kuuzia bidhaa zao.“hata kama mjasirimali mwanamke ukimpa mtaji wa biashara na mafunzo changamoto kubwa ni kupata eneo la kuweza kuuza hiyo bidhaa yake aliyotengeneza kwa mikono yake mwenyewe,” amesema Mrema
Pichani
juu na chini ni Baadhi ya Wajasiriamali Wanawake wakifuatilia hotuba ya
mwenyekiti wa TANCRAFT Bi. Elihaika Mrema alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari katika jengo la Biashara la DAR FREE MARKET lililopo
barabara ya Ali Hassan Mwinyi karibu na Ubalozi wa Kenya nchini.
Amesema kuwa Tancraft ni chama cha wajasirimali wanaotengeneza bidhaa kwa kutumia mali ghafi za kutoka nchini kama vile nguo za batik, vikapu, minyaa, vitu vya ufinyanzi,vinyago, shanga, bidhaa za ngozi, chakula na usindikaji wa aiana zote zikiwemo asali.
Hii
ni moja ya zawadi ya kikombe kwa Chama cha Wajasiriamali Wanawake
Tanzania (TANCFRAFT) walichowahi kupata kwa kuonyesha bidhaa zenye ubora
wa kimataifa.
No comments:
Post a Comment