EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, February 19, 2014

MTWARA HALI YA MVUA YALETA KIZAAZAA WANANCHI WABAKI BILA MAKAZI HUKU WENGINE WAKIPOTEZA MALI ZAO



HALI YA SOKO KUU MTWARA IKO HIVI

NA:VERONICA VICTOR
Mvua zinazoendelea kunyesha Mkoani Mtwara zimesababisha baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, kupoteza makazi yao na kusababisha usumbufu mkubwa unaotokana na maji kujaa katika nyumba zao.

Aidha mvua hizo zimefanya wananchi hao kupoteza vyakula na mali, huku  wafanyabiashara nao wakiwa katika wakati mgumu baada ya biashara zao na maeneo wanayofanyia biashara hizo kuingiliwa na maji.
Mwandishi wa habari wa pride fm alijionea hayo leo asubuhi wakati alipotembelea maeneo yaliyoathirika ya magomeni bomba la bure, chuno na soko kuu katika Manispaa ya Mtwara.
SOKO LA MBOGAMBOGA MTWARA
 Wakizungumza na mwandishi huyo kwa nyakati tofauti wakazi wa magomeni bomba la bure wamesema kuwa tatizo la maji kujaa limesababishwa na ujenzi wa barabara, lilipowekwa kalavati lenye tundu dogo linaloshindwa kupitisha maji kwa urahisi,  na sababisha maji hayo kujaa na kuingia katika nyumba za watu.
MAENEO YA MAKAZI YA WATU

 
Aidha kwa upande wa mwenyekiti wa soko kuu la Manispaa ya mtwara Bw Ramandhani  licheta, amekiri kuwa hali ya soko  hairidhishi hususani eneo linalotumika kwa biashara za mboga na matunda, kwa kuwa halina uwezo wa kutoa maji yatokanayo na mvua.
HALI NDIYO HII

No comments:

Post a Comment