EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Sunday, January 19, 2014

Viongozi wa kisiasa waonywa kuitumia TAHLISO

MWENYEKITI mstaafu wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taaluma za Juu Tanzania (TAHLISO), Amon ChakushemeireMWENYEKITI mstaafu wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taaluma za Juu Tanzania (TAHLISO), Amon Chakushemeire, amesema jumuiya hiyo inaendeshwa kitaaluma na si kisiasa.
Chakushemeire aliyasema hayo juzi jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhi nafasi hiyo kwa mwenyekiti mpya wa TAHLISO, Moses Mdee, na kueleza kuwa viongozi wa kisiasa wanapaswa kuacha kuitumia jumuiya hiyo kwa lengo la kujinufaisha.
Alisema kuwa wapo baadhi ya wanasiasa wanaotaka kuwania nafasi za juu za uongozi wamekuwa wakiingilia majukumu ya kiuongozi ya jumuiya hiyo.
“Wapo wanasiasa wanaotarajia kugombea urais mwaka 2015 wanaingilia uongozi wa TAHLISO kwa utashi wao ili iendeshwe kisiasa, hali iliyosababisha kutaka kuingiza usiasa na kutuletea wagombea wao katika uchaguzi uliofanyika mwaka jana,” alisema.
Chakushemeire alisema licha ya jumuiya hiyo kutegemea taasisi za nje katika kujiendesha, lakini katiba yao hairuhusu kushirikishwa wanasiasa ikiwemo kusaidiwa na taasisi zinazojiendesha kisiasa.
Alisema changamoto inayoikabili TAHLISO ni wimbi la wanafunzi wa elimu ya juu kugubikwa na siasa badala ya kuweka malengo katika elimu itakayowanufaisha kwa maisha yao ya baaadae.
“Ni jambo la kusikitisha kuona elimu yetu sasa ni uwanja wa siasa, wanasiasa wengi wanawatumia wanafunzi wa elimu ya juu kujinufaisha kisiasa ikiwa ni pamoja na kupiga kampeni za siri siri,” alisema.
SOURCE: TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment