EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, January 30, 2014

SOKO MTWARA LAKOSA HUDUMA MUHIM



NA: /Mohamedi,Zawadi & Majidu.
 Wafanyabiashara wa  Soko la Kiyangu mkoani Mtwara wameiomba serikali kuboresha na kuweka huduma muhimu katika soko hilo, ikiwepo pamoja na huduma ya choo, maji, umeme na usafi. 
Hayo yamesemwa  mapema hii leo na wafanyabiashara wa soko hilo wakati wakizungumza na Mwandishi wa Habari wa Pride Fm Redio, walipokuwa  wanatoa kero zao kuhusiana na soko hilo.
Mmoja wa wafanyabiashara hao Bi Somoe Hamisi, amesema kuwa kumekuwepo na tatizo la ukosefu wa choo kwa muda mrefu katika soko hilo ,ambapo inapelekea wafanyabiashara hao kujisaidia katika maeneo ya soko hali ambayo inahatarisha afya zao.
Aidha Bi Asha Bakari na Dayness Muhaja wametaja matatizo mengine  kuwa ni pamoja na ukosefu wa umeme na maji katika soko hilo kongwe, na kulalamikia hali ya usafi kuwa ni mbaya na kupelekea wafanyabiashara wengi kuhamia katika masoko mengine.
Wafanyabishara hao wametoa wito kwa serikali na uongozi wa Manispaa kushughulikia kwa haraka tatizo la ukosefu wa choo ili kunusuru afya zao pamoja na wateja wa bidhaa katika soko hilo.
                                                    

No comments:

Post a Comment