EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, January 16, 2014

KUTOKA LONDON: Manchester United itajinusuru kama itamfukuza Moyes



 

MMEKUWA watu wa aina yake na zawadi nzuri katika maisha yangu, lakini sasa kazi yenu ni kumuunga mkono kocha wenu mpya.”
Hayo yalikuwa maneno ya kocha, Alex Ferguson, aliyoyatamka pale Old Trafford katika hotuba yake ya kuwaaga wachezaji na klabu ya Manchester United mwishoni mwa msimu uliopita. Ilikuwa ni baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka 27.
Wote – wachezaji, viongozi na washabiki walionekana kumuunga mkono kwa dhati kocha mpya, David Moyes.
Kweli msimu ukaanza, Manchester United ikaifunga Swansea, lakini mashabiki wakaonekana kuwa naye hata katika shida pale Manchester City ilipowakung’uta mabao 4-1 na pia walipopigwa mfululizo na Everton na Newcastle.
Hadi Ijumaa ya wiki iliyopita hali ya hewa ilikuwa imechafuka Old Trafford kwani Mashetani Wekundu walikuwa wamekubali vipigo vitatu mfululizo.
Katika maanguko yao, Mashetani Wekundu wamekuwa wakisema kwamba hakuna tatizo kwani watarudi katika kiwango na kusonga mbele na ushindi.

Hata hivyo, baadhi ya wadau wameanza kupata hisia na mawazo tofauti juu ya klabu, baada ya kujiuliza tatizo lipo wapi wakati kikosi ni kilekile cha msimu uliopita alichokiacha Ferguson?
Tena kuna nyongeza ya Wilfred Zaha aliyekuwa ameachwa kwa mkopo Crystal Palace baada ya kusajiliwa na kocha huyo aliyepita.
Sasa kuna wanaodai tatizo lipo kwa kocha Moyes na kwamba kama wanataka kurudi juu katika nafasi walizozizoea, lazima wachukue uamuzi mgumu kwa kumwondosha kwa madai kwamba hakuwa chaguo sahihi.
Je, Bodi ya Wakurugenzi ya Manchester United itakaa na kukiri kwamba walifanya makosa kukubali ushauri wa Ferguson kwa kumteua Mskochi mwenzake, kisha wamwite Moyes, wamshukuru kwa ‘jitihada’ zake na kuachana naye?
Baadhi ya takwimu zinawashitua mashabiki wa Manchester United na wadau wengine wa soka, kwa sababu katika miaka 27 ya ukocha wa Ferguson ni mara moja tu timu hiyo ilitolewa katika raundi ya tatu ya Kombe la FA, lakini Moyes katika miezi yake sita ameshatolewa tayari katika raundi hiyo.
Swansea ilitia doa historia ya Manchester United maana ushindi wake wa Januari 5 ndio wa kwanza kuupata Old Trafford tangu timu hiyo  ilipoanzishwa.
SOURCE: MWANASPORT

No comments:

Post a Comment