EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Sunday, November 10, 2013

PAUL KAGAME AICHANGANYA AFRIKA



Pamoja na nchi ya Rwanda kuwa katika shinikizo la kimataifa, kuhusu tuhuma za kuwafadhili waasi wa kundi la M23 waliokuwa wakipambana na serikali ya DRC, nchi hiyo imeendeleza ukimya wa hali ya juu tangu kushindwa kwa kundi hilo.
 
Rais Paul Kagame wa Rwanda
Mapema siku ya Jumanne kundi hilo lilitangaza kuhitimisha miezi 18 ya uasi wake, baada ya kushindwa vibaya na kuangukia mikononi mwa majeshi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC) wakisaidiwa na kikosi maalumu cha Umoja wa Mataifa.
Kwa sasa waasi hao wako chini ya shinikizo la kusaini rasmi makubaliano ya amani kesho Jumatatu nchini Uganda, nchi ambayo wapiganaji wengi wa kundi hilo, wamekimbilia huku idadi kubwa ya wapiganaji waliojeruhiwa wamekimbilia nchini Rwanda.
Wataalam wa Umoja wa Mataifa wamekuwa wakiishutumu kwa kuwaunga mkono kwa kiasi fulani waasi hao, licha ya mataifa hayo kukanusha vikali madai hayo.

No comments:

Post a Comment