Naibu Raisi wa Kenya-William Ruto |
Naibu Rais wa Kenya William Ruto amewaambia
waandishi wa habari mjini The Hague nchini Uholanzi anakohudhuria vikao vya
kesi dhidi yake kuwa, ataendelea kuhudhuria vikao hivyo huku Kenya ikisubiri
maamuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kutoa maamuzi juu ya kuahirishwa
kwa kesi dhidi yake na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta.
Ruto alitumia maneno makali dhidi ya waendesha mashtaka wa mahakama ya ICC akisema imebainika wazi kuwa utendaji kazi wao ulikuwa hovyo, na kwamba waliwashawishi mashahidi kwa kuwapa hongo ili kutoa ushahidi wa uwongo dhidi yake na washtakiwa wenzake.
Ruto alitumia maneno makali dhidi ya waendesha mashtaka wa mahakama ya ICC akisema imebainika wazi kuwa utendaji kazi wao ulikuwa hovyo, na kwamba waliwashawishi mashahidi kwa kuwapa hongo ili kutoa ushahidi wa uwongo dhidi yake na washtakiwa wenzake.
Mwishoni mwa wiki viongozi wa Umoja wa Afrika katika mkutano maalum mjini Addis Ababa, Ethiopia walitoa mwito kwa Baraza la Usalama kufikia azimio litakaloahirisha kwa mwaka mmoja kesi dhidi ya viongozi hao wa Kenya.Viongozi hao wa Afrika walimshauri Rais Kenyatta kutohudhuria vikao vya kesi dhidi yake vinavyotarajiwa kuanza Novemba 12 huko The Hague katika mahakama ya kimataifa –ICC.
No comments:
Post a Comment