EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, August 14, 2014

NDANDA FC YAICHAPA JKT RUVU 4-0

NA MSHAMU NGOJWIKE
TIMU  ya Ndanda Fc, jana ilianza vyema michezo yake ya kirafiki baada ya kuifunga JKT Ruvu kwa mabao 4-1,kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Ardhi jijini  Dar es Salaam.

Ndanda Fc imeweka kambi ya siku 40 katika Chuo Kikuu Cha Ardhi jijini,Dar es Salaam,ikiajiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bara mwaka huu.
DENIS KITAMBI KOCHA NDANDA FC

Mchezo huo wa kujipima ubavu, ulikuwa wa kuonyeshana ufundi huku kila kocha akitumia vikosi viwili ili kutambua ubora wa timu yake.

Lakini Ndanda Fc walionekana kuukamia  mchezo huo, baada ya kuonyesha kandanda safi na pasi za kuonana,kupitia kwa wachezaji wao waliowasajili msimu huu.


Mabao ya Ndanda Fc yalifungwa na Jacob Masawe,Nassoro Kapama,Rajabu Isihaka na Mshambuliaji Mnigeria Lukman Abegunrin,huku la JKT Ruvu lilifungwa na Saidi Dihile.

Akizungumza na SWACOTZ FORUM,Kocha Msaidizi wa Ndanda Fc, alisema kuwa amefurahishwa na uwezo walioonyesha wachezaji kwenye mchezo wa leo,na atatumia fursa  ya kurekebisha makosa aliyoyaona katika mchezo huo.

“Wachezaji wamecheza Vizuri hata kama kuna mapungufu madogo madogo ambayo nitakaa na kuyatafutia ufumbuzi kabla ya kucheza mechi nyingine ya kirafiki,”alisema.

Alisema kuanzia wiki ijayo watatumia muda mwingi wa kucheza mechi za kirafiki na timu ambazo zinashiriki Ligi kuu Tanzania Bara,ili kukitambua vizuri kikosi chake.



No comments:

Post a Comment