EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, May 26, 2014

SIMBA SASA UCHAGUZI HALALI KAMATI YAMALIZA KAZI


DKT NDUMBARO
Kamati ya uchaguzi ya klabu ya Simba, leo itakutana na waandishi wa habari kutangaza matokeo ya mapigamizi. Kamati hiyo hiyo ya mwanasheria maarufu, Dkt Damas Daniel Ndumbaro, imekaa na kusikiliza mapingamizi yote na leo ndiyo majibu.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Simba, kila kitu kilikamilika jana na leo ni siku ya kutangaza.
“Kamati itakutana na waandishi saa saba na nusu mchana pale ofisi za TFF kwa ajili ya kutangaza,” kilieleza chanzo.
Kati ya waliokuwa wamekatiwa rufaa ni wagombea wa nafasi ya urais, Michael Wambura na Evans Aveva.
Lakini pia baadhi ya wagombea ambao walikuwa kwenye kamati ya utendaji ya Simba katika uongozi uliopita.

No comments:

Post a Comment