EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, March 6, 2014

FISTULA YAICHANGANYA TANZANIA WANAWAKE 200000 WAATHIRIWA NA GONJWA HILO



Dar es Salaam. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imesema kuwa takwimu zinaonyesha kwamba wanawake 20,000 nchini wanaishi na ugonjwa wa Fistula.
Hayo yamo katika hotuba ya Mke wa Rais, Salma Kikwete aliyoitoa kwenye hafla iliyowakutanisha wanawake mashuhuri nchini iliyofanyika Dar es Salaam.
“Licha ya ugonjwa wa fistula kutibika kirahisi, kutokuwapo kwa ufahamu, umaskini na unyanyapaa vimekuwa ni kikwazo kwa wengi kutibiwa,” alisema Mama Salma.
Salma aliipongeza Kampuni za Simu za Mkononi za Vodacom na Hospitali ya CCBRT kwa kuwakomboa wanawake wenye ugonjwa huo. A lisema kwa msaada wa kampuni hiyo na CCBRT, imepanua huduma zake kwa kuongeza vituo vingine vya afya Tanzania na hivyo kuwafikia wanawake wengi zaidi.
“Jamii za kimataifa zimegundua kuwa, kuna faida kubwa kama tutaziba pengo la kijinsia lililopo katika masuala ya afya kwa kuwapatia wanawake uhuru ili waweze kuishi maisha ya furaha,” alisema.
Naye Mkuu wa Idara ya Vodacom Foundation, Laura Turkington alisema tangu huduma ya ujumbe na matibabu yaani text to treatment utambulishwe mwaka 2010, zaidi ya wanawake 1,900 wamefaidika na kufanyiwa operesheni ya fistula.
Alisema operesheni hiyo ilibadilisha maisha ya wanawake na waliweza kufanya kazi zao na kuishi maisha yenye furaha.
“Leo hii ninavyozungumza Taasisi ya CCBRT ni kituo kikubwa duniani cha matibabu ya ugonjwa wa fistula, kwa misaada kutoka kwa Serikali za Uswisi na Uholanzi pamoja na Kampuni ya Vodafone Foundation,” alisema.

No comments:

Post a Comment