Meneja huyo, ambae ndie Msimu wake wa
kwanza Old Trafford baada kurithi nafasi ya Sir Alex Ferguson ambae
alistaafu Mwezi Mei baada ya Miaka 26, amekuwa na mwanzo mbovu na Man
United, ambao ndio Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, wapo Nafasi ya
7 kwenye Ligi na wameshuhudia vipigo vitano Old Trafford tangu Moyes
atwae hatamu.
Katika Barua hiyo, Moyes ameandika:
“Ingawa nilijua kazi hii ni changamoto kubwa wakati naichukua, Msimu huu
mgumu sio kitu nilichofikiria kama nyinyi Mashabiki ambavyo sasa
mnafikiria, na sasa Wachezaji wangu, Wafanyakazi na mimi tutahaha kulipa
fidia kwa hilo.”
“Nyinyi mmezoea kuona mafanikio
Manchester United na sapoti mliyowapa Wachezaji na mimi Msimu huu wote
hauna mfano. Nje ya Nyumbani Mashabiki wanaosafiri na Timu wamekuwa bora
kuliko wote Nchi nzima na hapa Old Trafford hamyumbi na tunafarijika
sana.”
“Kusapoti Timu yako ikiwa inashinda ni
kitu rahisi lakini ni ngumu mno ikiwa mambo yanaenda kombo na uzalendo
wenu mlioonyesha hauna kifani.”
Moyes aliendelea kwa kutamka uhakika
wake kwamba: “Kila kitu tulichopitia kitatuimarisha zaidi, kuifanya Timu
imara na Klabu bora baadae. Kwa Miaka mingi mmeona Vikosi imara
vikishinda hapa, na, katika muda, nina hakika kabisa tutaona Vikosi
imara vikishinda tena hapa.”
MAN UNITED-Mechi zijazo 4:
[Ligi Kuu England isipokuwa inapotajwa]
Machi 8 West Bromwich v Man United
Machi 16 Man United v Liverpool
Machi 19 Man United v Olympiacos [UEFA CHAMPIONZ LIGI]
Machi 22 West Ham v Man United
No comments:
Post a Comment