Ndege za kivita za Pakistan zilishambulia maeneo ya kaskazini magharibi mwa nchi hiyo maeneo yanayoshukiwa kuwa ngome na maficho yakundi la Taliban .
Mashambulizi hayo katika Jimbo la Waziristan yanatizamwa na wandani wa maswala ya Mashariki ya mbali kama njia ya jeshi la taifa kulipiza kisasi shambulizi lililosababisha vifo vya wanajeshi kadhaa mapema wiki hii.
Mapema juma hili muafaka wa amani uliokuwa ufanyike kati ya serikali na wapiganaji wa Taliban yalisambaratika baada ya kundi moja linalounga mkono Taliban, kusema kuwa limewauwa wanajeshi 23 waliokuwa wamewateka.
Ripoti kutoka mji wa Mir Ali zinasema kuwa wapiganaji wa kigeni ni miongoni mwa wale waliouawaa katika mashambulizi haya ya usiku Kucha.
No comments:
Post a Comment