EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, February 27, 2014

REAL MADRID YAFANYA KUFULU UEFA JANA SCHAKLA 04 WAPEWA KICHAPO CHA PAKA MWIZI

KIUNGO REAL MADRID GALETH BALE AKIJARIBU KUIPITA NGOME YA SCHLAKE 04
VIGOGO wa Spain, Real Madrid, wapo mguu mmoja ndani ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI baada ya kuibonda Schlake 04 Bao 6-1 huko Veltins Arena Jijini Gelsenkirchen Nchini Germany katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano Timu 16.

Wakicheza Ugenini huko Veltins Arena Jijini Gelsenkirchen Nchini Germany, Real Madrid walishinda Mechi hii ya Kwanza ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, Raundi ya Mtoano Timu 16, kwa kuichapa Schalke Bao 6-1 na hadi Mapumziko walikuwa mbele kwa Bao 2-0.

Bao la kwanza lilifungwa Dakika ya 13 kwa kazi njema ya Gareth Bale aliempa Cristiano Ronaldo aliepiga kwa kisigino na Mpira kuguswa na Beki Santana na kumfikia Karim Benzema alieipa Real Bao.
Bao la Pili lilifungwa Dakika ya 21 na Gareth Bale baada ya kazi nzuri ya Benzema na Bale kufunga.


Katika Dakika ya 52, pasi ya Bale ilimfikia Cristiano Ronaldo ambae alimhadaa Joel Matip na kisha kufunga Goli kwa shuti la Mguu wa kushoto.
Dakika ya 57, Benzema akafunga Bao lake la pili na la 4 kwa Real kufuatia pasi ya Ronaldo ya kisigino na katika Dakika ya 69 Bale pia akafunga Bao lake la Pili na la 5 kwa Real baada kupokea pasi ya Sergio Ramos.
Nae Ronaldo haukuachwa nyuma kwa kufunga Bao 2 kwani katika Dakika ya 89 alipiga Bao baada Kiungo wa Schalke Leon Goretzka kunyang'anywa Mpira na Isco aliempa Karim Benzema aliempenyezea Cristiano Ronaldo na kuandika Bao la 6.
Schalke walifunga Bao lao pekee katika Dakika ya 90 Mfungaji akiwa Klaas-Jan Huntelaar.
VIKOSI:
Schalke: Fahrmann; Howedes, Matip, Felipe Santana, Kolasinac; Boateng, Neustadter; Farfan, Meyer, Draxler; Huntelaar
Akiba: Hildebrand, Hoogland, Goretzka, Papadopoulos, Obasi Ogbuke, Fuchs, Szalai.
Real Madrid: Casillas; Carvajal, Pepe, Sergio Ramos, Marcelo; Modric, Alonso, Di Maria; Bale, Benzema, Ronaldo
Akiba: Diego Lopez, Varane, Fabio Coentrao, Arbeloa, Jese, Isco, Illarramendi.
Refa: Howard Webb [England]
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
MARUDIANO
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
[Saa za Bongo]
Jumanne Machi 11
22:45 Bayern Munich v Arsenal FC [2-0]
22:45 Atletico de Madrid v AC Milan [1-0]
Jumatano Machi 12
22:45 FC Barcelona v Manchester City [2-0]
22:45 Paris Saint-Germain v Bayer 04 Leverkusen [4-0]
Jumanne Machi 18
22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü [1-1]
22:45 Real Madrid CF v Schalke 04 [1-6]
Jumatano Machi 19
22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg [4-2]
22:45 Manchester United v Olympiacos CFP [0-2]

No comments:

Post a Comment