EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, January 16, 2014

Ukikamatwa na jezi feki za Mbeya City umekwisha

Mashabiki wa timu ya Mbeya City wakiishangilia timu yao. Picha na Maktaba 

0
Share
WAJANJA kaeni chonjo! Mbeya City imetangaza vita kwa kuanzisha msako mkali wa wafanyabiashara wanaouza jezi na bidhaa zenye rangi na nembo zake.
Muda mfupi baada ya kuonekana ina mafanikio katika Ligi Kuu Bara, jezi na skafu za Mbeya City zimekuwa zikiuzwa kwa wingi katika miji mbalimbali nchini bila timu hiyo kunufaika.
Kutokana na hali hiyo, klabu hiyo inayomilikiwa na Halmshauri ya Jiji la Mbeya, imeweka watu wake maalumu wanaozunguka mitaani katika majiji mbalimbali kuwabaini watu wanaouza bidhaa zenye nembo yao bila makubaliano maalumu.
Akizungumza na Mwanaspoti, Ofisa Habari wa Mbeya City, Fred Jackson alisema wameweka mkakati huo baada ya kubaini kuwepo kwa watu wachache wanaonufaika na jina la klabu hiyo huku wao wakiwa hawanufaiki.
“Kuna watu wanauza jezi zenye nembo yetu ambayo ni alama ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya jambo ambalo ni hatari kwani wanaonufaika ni wao na si sisi ambao tunaihudumia timu kwa kila hali.
“Kuanzia sasa mtu tutakayemkamata anauza bidhaa hizo tutampeleka mahakamani ili akakumbane na sheria maana huo ni wizi wa wazi,” alisema Fred kwa msisitizo.
Wafanyabiashara mbalimbali hapa nchini wamekuwa na tabia ya kutengeneza jezi zenye nembo za klabu mbalimbali za ligi kuu na kuziuza bila ya makubaliano yoyote na viongozi wa timu hizo.
SOURCE:MWANASPORT

No comments:

Post a Comment