TIMU ya taifa ya
Ufaransa inatarajiwa kuchezwa mechi tatu za kimataifa za kirafiki kabla
hawajaondoka kuelekea nchini Brazil kushiriki michuano ya Kombe la
Dunia.
Shirikisho la Soka la nchi hiyo limedai kuwa timu hiyo itacheza
mchezao wake wa kwanza wa kirafiki huko Stade de France mei 27 huku
michezo mingine ikichezwa katika miji ya Nice Juni mosi na Lille Juni
8.
Majina ya timu watakazopimana nazo nguvu yanatarajiwa kutolewa mapema
mwakani. Ufaransa imepangwa kundi F sambamba na timu za Switzerland,
Ecuador na Honduras.
PETROVA AJITOA AUSTRALIA OPEN.
MCHEZAJI nyota wa
tenisi, Nadia Petrova wa Urusi amejitoa katika michuano ya wazi ya
Australia inayotarajiwa kuchezwa mapema mwakani kufuatia kifo cha mama
yake kilichotokana na ajali ya gari.
Mama yake Petrova aitwaye Nadezhda
Illyina alikuwa mwanariadha ambaye aliwahi kushinda medali ya shaba
katika mbio za mita 400 kupokezana vijiti katika michuano ya olimpiki
iliyofanyika jijini Montreal mwaka 1976.
Mrusi mwenzake Maria Kirilenko
ambaye anashika namba 19 katika orodha za ubora duniani naye amjitoa
kutokana na majeruhi.
Kujitoa kwa Petrova kunamaanisha kuwa Tsevetana
Pironkova mwenye umri wa miaka 26 raia wa Bulgaria atachukua nafasi hiyo
katika droo kubwa ya michuano hiyo.
No comments:
Post a Comment