EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, November 6, 2013

NIGERIA YASISITIZA TATIZO LA ICC NA NCI ZA AFRIKA KUWA MAREKEBISHO NI LAZIMA



Nigeria imetaka kufanywa marekebisho katika muundo wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC). 
 
Rais-Gudluck Jonathan wa Nigeria
Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria amesisitiza juu ya ulazima wa kufanyiwa marekebisho muundo wa mahakama ya ICC, na kueleza kuwa nchi yake haitajiondoa katika chombo hicho cha kimataifa, licha ya nchi za Kiafrika kubainisha wasiwasi wao kuhusu utendaji wa mahakama hiyo.
Rais wa Nigeria ameongeza kuwa nchi yake itafanya juhudi kwa kushirikiana na nchi nyingine ili kuiimarisha mahakama ya ICC.
Rais Goodluck Jonathan ambaye aliyasema hayo huko Abuja mji mkuu wa Nigeria, wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai yenye makao yake huko Hague Uholanzi, ameongeza kuwa mahakama hiyo inapaswa kutafuta ufumbuzi wa masuala mbalimbali na si kuyafanya masuala hayo kuwa magumu zaidi.
Rais Goodluck Jonathan amesema mahakama ya ICC inapasa kutambua matatizo ya viongozi wa nchi za Kiafrika na kutilia maanani wasiwasi wa viongozi hao.

No comments:

Post a Comment