EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, November 6, 2013

M23 YAJISALIMISHA YATAKA AMANI CONGO



Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo linapanga kupambana sasa na waasi wa Kihutu kutoka Rwanda walioko  katika  eneo  la mashariki  mwa  nchi  hiyo.  


Msemaji  wa  serikali  ya  Kongo amesema hayo leo na  kuongeza  kuwa  hakuna  nafasi  tena  nchini humo  kwa  jeshi  ambalo si rasmi.
Mende  amesema  kuwa   kundi la  waasi  la  M23  ambalo  limeshindwa,  limekuwa  katika  orodha ya  juu  kabla  ya  kusalimu amri  leo.
Mende  amesema  kuwa  nafasi  ya  kundi  hilo  imechukuliwa  sasa na  kundi  la  waasi  la  FDLR , na   sasa  ni  zamu  ya kundi  hilo kunyang'anywa  silaha.Msemaji  huyo  wa  serikali  amesema  kuwa hatua  za  kijeshi  zitachukuliwa  katika  mapambano  ambayo yatafanywa  na  jeshi  la  nchi  hiyo,  dhidi  ya  vikundi  mbali  mbali vyenye silaha  katika  eneo  la  mashariki  ya  nchi  hiyo.

Mende amesema  kuwa  ushindi  wa  jeshi  la  Kongo  linalosaidiwa  na kikosi  maalum  cha  jeshi  la  Umoja  wa  Mataifa,  dhidi  ya  kundi  la waasi  lililokuwa  na  wapiganaji  wengi  wa  kabila  la  Watutsi  la M23, haufikishi  mwisho juhudi  za  kurejesha  usalama  katika  nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment