EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Wednesday, November 6, 2013

CHINA YAPATA JARIBU-OFISI KUU ZA CHAMA TAWALA CHA KIKOMUNISTI CHALIPUKA NA MMOJA AFARIKI



Kumekuwepo na misururu ya milipuko midogo nje ya ofisi za kimkoa za chama tawala cha Kikomunisti nchini China na kusababisha kifo cha mtu mmoja 


Maafisa wa polisi katika eneo hilo wamesema kuwa milipuko hiyo ilisababishwa na mabomu madogo yaliyotengenezwa nyumbani.
Mlipuko hiyo iliotokea muda wa asubuhi wenye shughuli nyingi, ilisababisha kuvunjika kwa madirisha na moshi mkubwa kufuka.
Ripoti zilizotolewa na shirika la habari la serikali zilisema kuwa mabomu madogo yalikuwa yamefichwa ndani ya maua kando ya barabara.
Milipuko hiyo imetokea Kaskazini mwa China katika eneo la, Tai-yuan, mkoani, Shanxi,Taarifa za vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa watu 8 wamejeruhiwa na magari mawili kuharibiwa.

No comments:

Post a Comment