EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Saturday, October 19, 2013

WAFANYA BIASHARA NA WAWEKEZAJI KUMIMINIKA MTWARA



Kufuatia ugunduzi wa mafuta na gesi katika mikoa ya kusini ya Lindi na Mtwara, serikali imewaalika wafanyabishara na wawekezaji kutoka nchini Finland, kuja kuwekeza hapa nchini hususani katika mikoa hiyo, ili kuweza kutoa fursa ya kukua kiuchumi kwa wananchi wa mikoa ya kusini.
 
George Mkuchika Waziri ofisi ya Raisi Utawala bora
Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora George Mkuchika, wakati akizungumza na mabalozi wa Finland Afrika, katika maadhimisho ya miaka 40 ya ushirikiano kati ya Finland na mikoa ya Lindi na Mtwara, sherehe zilizofanyika katika ukumbi wa Veta Mjini Mtwara.



Amesema kuwa uwekezaji huo unaweza kufanyika katika maeneo ya uzalishaji wa umeme, viwanda, usafirishaji, kilimo, madini, miundombinu, ambapo amesema kuwa kwa kufanya hivyo wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara nao watapata fursa za kupata ajira na kujiongezea kipato na hivyo kujinasua na lindi la umasikini.
Mkuchika amesema kuwa misaada ya serikali ya Finland imekuwa ikilenga katika sekta  tatu za ushirikiano ikiwemo sekta ya uvuvi, mazingira na kilimo na kusaidia bajeti ya Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Waziri huyo amesema kuwa katika maeneo yote hayo ya sekta za ushirikiano, mkazo mkubwa umewekwa katika kupunguza umasikini na kuimarisha demokrasia, utawala bora, utawala wa sheria na sera endelevu za maendeleo katika misingi ya umoja wa mataifa ya malengo ya maendeleo ya millennia.
Awali akizungumza katika sherehe hizo za miaka 40 ya ushirikiano kati ya Finland na Mikoa ya Lindi na Mtwara, kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara Ludovick Mwananzila, ambaye ni mkuu wa mkoa wa Lindi amesema kuwa hivi sasa fursa ni nyingi katika mikoa ya kusini kufuatia kufunguka kwa miundo mbinu ya barabara na hivyo kufanya shughuli za kibiashara na za kiuwekezaji kuongezeka kwa wananchi.

No comments:

Post a Comment