"WAPIGWE TU" YA MIZENGO PINDA ITAMFIKISHA KORTINI

KAULI ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ya kubariki vyombo vya dola
kuendeleza kipigo kwa raia wanaokaidi amri imechukua sura mpya baada ya
Kituo cha Sheria na Haki za Bindamu (LHRC) kutangaza kumburuza
mahakamani wiki hii kutokana na kushindwa kufuta kauli yake.
Juni 20, mwaka huu, wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo bungeni,
Waziri Mkuu, Pinda, alivitaka vyombo vya dola kuendelea kuwapiga raia,
akisema kuwa hakuna namna nyingine kwani serikali imechoka.
Kauli hiyo imekuwa ikipingwa na wananchi, mashirika ya kutetea haki za
binadamu na wanasiasa wakimtaka Waziri Mkuu, Pinda, kuifuta kwa kuomba
radhi, wakidai kuwa inachochea...
MBUNGE WA CCM ANAYEDAIWA KUFADHILI MADAWA YA KULEVYA AJISALIMISHA POLISI

Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, jijini Dar es Salaam kwa tiketi ya CCM,
Iddi Azzan, aliyetajwa kwenye barua inayosadikiwa kuandikwa na wafungwa
Wakitanzania waliopo Hong Kong “amejilisalimisha” kwenye ofisi za jeshi
la polisi na kulitaka jeshi hilo lifanye uchunguzi dhidi ya tuhuma
zilizoelekezwa kwake, ili hatua nyingine na ikibidi sheria, vichukue
mkondo wake.Azzan amesema alienda mwenyewe kutoa taarifa katika Kituo Kikuu cha Polisi Kati, jijini Dar es Salaam."Nimeamua
kwenda kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa taarifa ili ufanyike
uchunguzi wa jambo hilo na ukweli ubainike na hatua za kisheria zifuate
juu yangu," alisema Azzan...
KAHABA APEWA KICHAPO NA MALAYA WENZAKE KWA KOSA LA KUJIUZA KWA BEI YA HASARA NA MKOPO

KAHABA mmoja katika mji wa Naivasha, jimbo la Rift Valley nchini
Kenya
amenusurika kufa baada ya kupewa kichapo kikali na makahaba wenzake
wakimtuhumu kujiuza kwa bei ndogo na kuwaharibia soko.
Wenzake hao wenye hasira walimtwanga kahaba huyo kwa ngumi
wakimshutumu kwa kutokuwa na ushirikiano na kuwaharibia soko hasa
ikizingatiwa kuwa hivi sasa ni kipindi cha mwisho wa mwezi
ambapo mahitaji ya kununua ngono huoongezeka.
Makahaba hao walitekeleza lengo hilo pale walipomzingira...
No comments:
Post a Comment