EBENEZA MARCH 9 2014
SWACO
royal
tt
NIMO
mvuto
Wednesday, November 26, 2014
staa wa bongo AUNT LULU HOI KITANDANI
Staa wa Filamu za Kibongo, Lulu Semagongo ‘Aunt Lulu’ yupo hoi kitandani baada ya kusumbuliwa na jino la juu ambalo anahofia kulitoa.
Akizungumza na Amani, Aunt Lulu alisema kuwa anajiona amekonda kwa maumivu ya jino tu na kutokana na vitisho anavyovipata kutoka kwa marafiki zake anaogopa kwenda kuling’oa.
“Yaani nina siku tatu sili nakunywa tu, vile vitu vigumuvigumu kama kuku na nyama za kuchoma navisikia kwa wenzangu kwani vinanishinda, nikitaka kuangua kilio niviweke mdomoni,” alisema Aunt Lulu.
Lulu alimalizia kwa kuwaomba mashabiki wake wamuombee kwani jino ni ugonjwa mdogo sana lakini kwake umekuwa ni mtihani mkubwa kwani kila akitaka kwenda kuling’oa anapatwa na hali ya woga.
SOURCE>>GLOBAL PUBLISHER
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment