EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Friday, May 23, 2014

SUAREZ ATHIBITISHA KUSHIRIKI KOMBE LA DUNIA



Luis Suarez anaamini kuwa atakua tayari kwa mwanzo wa michuasno ya kombe la dunia baada ya kupata maumivu ya goti na kufanyiwa upasuaji asubuhi ya siku nya jumatano yaani juzi.
Straiker huyo wa Liverpool na nchi ya Uruguay alikwenda kufanyiwa uchunguzi na taarifa zilieleza kuwa suerez kwa sasa anasaidiwa na kiti cha magurudumu kutembea ingawa  mwenyewe amenukuliwa akisema.

"Nitakua safi na imara katika siku chache zijazo na kwa asilimia 100 na nitaweza kuisaidia timu yangu ya taifa katika michuano ya kombe la dunia”.
Straika huyo mwenye umri wa miaka 27- ameweka picha yake kwenye ukurasa wake wa twiter akiwa na familia yake, pamoja na ujumbe unaosema: "Ahsante sana kwa jumbe za kuniunga mkono,upendo pamoja na kunipa moyo ndani ya siku hizi za majeruhi!
"Ni nguvu ambayo wapendwa wangu mnanipa/mnaionyesha kwangu... watanifanya nifanye kazi kwa bidiii na kufanikiwa kushiriki kombe la dunia hii ni kwa familia yangu na watu wote mnaonisapoti!!"
Suarez alifanyiwa upasuaji baada ya kutojisikia vizuri katika goti lake wakati wa mazoezi akiwa na timu yake ya taifa ya Uruguay siku ya jumatano, na shirikisho la soka la Uruguay lilieleza kuwa maumivu aliyoyapata suarez yanatokana na mshituko alioupata wakati wa mechi za mwisho za michuano ya ligi kuu nchini uingereza dhidi ya Newcastle.

Timu ya taifa ya Uruguay itafungua michuano ya kombe la dunia kwa kucheza na timu ya taifa ya  Costa Rica tarehe  14 mwezi wa sita , na itafata mechi ya timu taifa ya uingereza na italy.
Wakati huohuo mlinzi wa timu ya Newcastle Paul Dummett, ambaye aliondolewa mara baada ya kumchezea rafu Suarez, amesema kuwa amepokea jumbe za lawama toka kwa washabiki wa Uruguay kupitia ukurasa wake wa twitter.
Akiongea na Mirror  Dummett, amesema: "Ni changamoto ambayo haiepukiki ni kweli alisababisha maumivu ya Suarez wakati walipokutana na akajaribu kuchukua mpira kwa mguu wake wa kushoto ndipo akaanguka chini.
"lakini akasema kuwa anatuma Suarez atashiriki michuano ya kombe la dunia akiwa na timu yake ya taifa  kwani yeye ni moja ya wachezaji muhimu na bora duniani hivyo anaamini atakua safi na atashiriki.

No comments:

Post a Comment