Ni wiki tatu zimepita tukishuhudia Eviction shows tatu zilizowapa
tiketi za kurudi makwao washiriki 6 mpaka sasa, na tumeshuhudia mshiriki
wetu Feza Kessy akiponea kwenye tundu la sindano baada ya kura za wa
Tanzania na wa Afrika kumuokoa, sasa ni zamu ya Nando ambaye yuko
hatarini wiki hii.
Big Brother jana ametaja majina ya washiriki 7 ambao wako hatarini
kutoka wiki hii na kati yao yupo kijana mpole, mtanashati, ‘handsome’
Nando anaeiwakilisha Tanzania, ikiwa ndio mara yake ya kwanza
kupendekezwa .
Washiriki wengine walipigiwa kura nyingi kutoka wiki hii ni love
birds Bolt na Betty, ambao hii si mara yao ya kwanza kupendekezwa...
KESI YA MENEJA WA MALAWI CARGO ANAYETUHUMIWA KUOMBA RUSHWA YA NGONO KWA MFANYAKAZI WAKE YAANZA KUUNGURUMA MAHAKAMANI
ALIYEKUWA
Meneja wa Kampuni ya Malawi Cargo tawi la Mbeya Evason Mwale(49) raia
wa nchi jirani ya Malawi, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mbeya
akituhumiwa kujihusisha na Rushwa ya Ngono.
Mwendesha
mashtaka wa Serikali Basilius Namkambe akisoma Mashtaka ya mtuhumiwa
huyo mbele ya Hakimu mkazi wa mahakama hiyo Gilbert Ndeuluo alisema
Mtuhumiwa anashtakiwa kwa makosa mawili ambayo ni Rushwa ya Ngono
kinyume cha kifungu cha 25 cha Sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa
namba 11 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2007.
Namkambe
alidai mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa anashtakiwa kwa kosa lingine la
matumizi mabaya ya...
BAADA YA NAPE KUITUHUMU CHADEMA, MBOWE NAYE AFUNGUKA NA KUDAI KUWA BOMU LILIRUSHWA NA FFU NA USHAHIDI ANAO
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe
amefichua siri kuhusu tukio la mlipuko wa bomu lililotokea jusi katika
viwanja vya Soweto, jijini Arusha.Katika kauli yake jana, Mbowe
ameibua tuhuma nzito dhidi ya Jeshi la Polisi, ambapo alidai kuwa askari
wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) ndiye aliyerusha bomu hilo.Akizungumza
na waandishi wa habari mjini hapa,baada ya kutembelea majeruhi katika
Hospitali ya Selian, Mbowe alisema chama chake kina ushahidi wa kutosha
juu ya askari huyo kurusha bomu.Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa
kambi ya upinzani bungeni,alisema wamefanikiwa kupata ushahidi wa
kutosha juu...
CATHY WA BONGO MOVIE ALIA NA USHIRIKINA ULIPO NDANI YA TASNIA HIYO....AWATAKA WASANII WAMRUDIE MUNGU
Mwigizaji wa Bongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’ naye amenyanyua kinywa chake na
kuonesha jinsi gani anakerwa na wasanii wanaoshinda kwa waganga ili
kutafuta ustaa.
Akiongea na mwandishi wetu hivi karibuni, Cathy alisema kuna baadhi
ya wasanii (hakuwataja majina) wamekuwa na tabia za kuzunguka kwa
waganga wakitafuta kuwa juu katika tasnia ya filamu suala ambalo
halipendezi na kuwasihi wawe na hofu ya Mungu.
“Vifo vya wasanii
vimetokea vingi sana, nilidhani kutokana na vifo hivyo wangepata hofu ya
Mungu na kuacha mambo yasiyofaa vikiwemo vitendo vya kishirikina lakini
hawakomi, wananikera sana. Ipo siku wataumbuka kwani...
KAULI YA SERIKALI KUHUSU KITITA CHA MILIONI 100 KWA MTU ATAKAYEMTAJA MTU ALIYERUSHA BOMU ARUSHA
Zifuatazo ni nukuu za maneno yaliyotolewa na Waziri wa nchi
Ofisi ya Rais, sera, uratibu na bunge William Lukuvi kuhusu hilo bomu
ambalo lililipuliwa kwenye mkutano cha Chadema Arusha.
“Mtu asiejulikana alirusha kitu katika kundi la watu
kilichosababisha mlipuko mkubwa, mkutano huu ulikua na ulinzi wa jeshi
la Polisi wakiwa na magari mawili… askari walisimama upande wa Kaskazini
ya uwanja ambapo mrushaji alikua mashariki na alirusha bomu kuelekea
Magharibi”
“Jaribio la Askari Polisi kutaka kumfata alierusha lilizuiwa
na makundi ya Wananchi ambao walianza kuwashambulia polisi kwa mawe na
kuwazomea na hivyo Polisi kulazimika...
MSHIRIKI WA TANZANIA ( FEZA KESSY ) AKIMUOGESHA MSHIRIKI WA ZIMBABWE ( HAKEEM) NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER
Video hizi hutolewa na big borther wenyewe kwa jamii kama sehemu ya
shindano hilo....
Wahiriki wote wa big brother wanajua ya kwamba jumba hilo limezingirwa
na kamera kila kona.Kwa hiyo, kama mtu ataamua kufanya ufuska au kukaa
uchi basi ajue kamera zitamrekodi na kumwanika hadharani....
Masharti hayo hujuzwa mapema kabla ya kuanza kwa shindano hilo...
Hakeem
Huyu ni mshiriki toka zimbabwe aliyepata bahati ya kuoga na dada yetu
Feza ndani ya bafu moja
Feza
Huyu ni mshiriki toka Tanzania....Yuko ndani ya afu moja akioga na
mshiriki wa Zimbabwe.....
Dakika chache baada ya kila mmoja kuoga...
VIDEO YA NAPE NNAYE AKIWAVAA CHADEMA NA KUDAI KUWA WANAHUSIKA NA MLIPUKO WA BOMU
Wakati jeshi la polisi na vyombo mbalimbali vya usalama vikihaha
kumtafuta mtu aliyerusha bomu katika mkutano wa kampeni huko Arusha
chama cha mapinduzi CCM kimetoa tamko kuhusiana na tukio hilo na
kukishutumu moja kwa moja chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema)
kuwa wao ndio wanaohusika na tukio hilo .
...
"MLIPUKO WA BOMU LA ARUSHA ULIPANGWA NA CHADEMA WENYEWE".....NAPE NNAUYE
Itakumbukwa tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa
madiwani kwa baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata
ishirini na mbili (22) -kati ya kata ishirini na sita (26)
zilizotangazwa kufanya uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.
Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha
kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa
na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na
asilimia 27.28%.
Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu
kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi
uliotukuka.
Hata...
...
No comments:
Post a Comment