EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Monday, February 17, 2014

WATOTO WATATU PEKEE NDIO WAMEJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MTWARA …………MKUU WA WILAYA ATANGAZA SIKU SABA KWA WAZAZI KUPELEKA WATOTO SHULE KABLA YA JUMATATU IJAYO KAMATAKAMATA KUANZA……...............................SIKILIZA ZAIDI HAPA CHINI....>>

 


MKUU WA WILAYA MTWARA MH: WILLIMAN KAPENJAMA NDILE.........PICHA NA MAKTABA
NA: KASSIM NGUMBI.............Mtwara


MKUU Wa Wilaya Ya Mtwara MH: Williman Kapenjama Ndile Ametangaza Siku Saba Kwa Wazazi Kupeleka Watoto Wote Waliofaulu Kujiunga Na Shule Za Sekondari Katika Wilaya Yake Kwenda Kuanza Muhula Wa Masomo Kabla Ya Hatua Za Kisheria Kuanza Kuchukuliwa Kwa Wazazi Watakaobainika Kutopeleka Watoto Hao Shuleni.Akizungumza Mapema Leo Asubuhi Kupitia Kipindi Cha Radio Cha Amka Na Pride Kinachorushwa Na Kituo Hiki Mh: Ndile Alisema Kuwa Mpaka Sasa Wilaya Bado Iko Nyuma Kielim Na Kwamba Kwa Mwaka 2014 Wanafunzi Wote Waliofaulu Mtihani Wa Darasa La Saba Ni Wanafunzi Watatu Tu Ndio Waliojiunga Na Kidato Cha Kwanza Kati Ya Wanafunzi Kumi Ya Hao.
Wakati Akitoa Maelezo Hayo Mkuu Huyo Pia Ametangaza Rasmi Siku Saba Za Kisheria Kwa Wazazi Kupeleka Watoto Walioko Mitaani Katika Shule Zao Walizofaulu Na Kwamba Wasipofanya Hivyo Mpaka Kufikia Jumatatu Ijayo Ya Tarehe 24 Wote Watafikishwa Mahakamani Kujibu Mashitaka Ya Kwa Nini Hawataki Kuwapeleka Watoto Wao Shuleni.
Aidha Katika Kutilia Mkazo Swala Hilo Mh: Ndile Amesema Kuwa Tayari Amekwishawaandikia Barua Za Amri Ya Kamatakamata Hiyo Watendaji Wote Na Maafisa Tarafa Wa Wilaya Yake Pamoja Na OCD Na Kwamba Jumatano Ya Wiki Hii Kutakuwa Na Kikao Kikubwa Cha Pamoja Kati Ya Ofisi Yake Na Maafisa Tarafa,Watendaji Na Polisi Wa Ngazi Ya Kata Kuzungumzia Juu Ya Hatua Alizozipanga.Mwisho Aliwataka Wanamtwara Kubadili Mawazo Ya Kuwa Elimu Ni Gharama Na Kwamba Lazima Waangalie Mazingira Yaliyopo Sasa Bila Ya Elimu Hakuna Kinachowezekana Na Kutoa Rai Kuwa Hata Kama Mtwara Fursa Zikaja Za Kutosha Kama Watu Wasipokuwa Na Sifa Ya Elimu Bado Wenyeji Watabaki Bila Kazi Na Kushindwa Kuzitumia Fursa Zilizopo Mkoani Na Ndani Ya Wilaya Zao.
MH:...NDILE
 Alisema Pia Hata Unapozungumzia Miaka Mitano Ijayo Mtwara Itakua Ndio Mji Unaoongoza Kwa Viwanda Na Uwekezaji Mkubwa Nchini Lakini Pasipo Elimu Tutabaki Kuwa Watazamaji Tu Na Ameeleza Kuwa Anasikitishwa Sana Na Hali Halisi Ya Watu Inapofikia Swala La Elimu Wengi Wanapeleka Watoto Serikalini Kuwa Ni Yatima Wakati Inapofika Katika Suala La Unyago Wanauwezo Wa Kuwahudumia Na Kuhudumia Gharama Za Ngoma Hizo Na Kwanini Washindwe Kwenye Swala La Elimu Pia Alisema Yeye Kama Mkuu Wa Wilaya Amekuwa Akijitahidi Sana Kutafuta Fursa Kwa Watu Wa Mtwara Ila Zinafeli Kutokana Namazingira Ya Elimu Ya Wahusika Kuwa Ndogo Kwa Mfano Mwaka Jana AMREF Ilitoa Pesa Zaidi Ya Shilingi Million Arobaini Kwa Wilaya Ili Waweze Kusomesha Watoto Waliopata  C Tatu Za Masomo Ya Sayansi Katika Fani Za Uganga Na Uuguzi Lakini Fedha Hizo Zilihamishwa Na Kupelekwa Bukoba Kwakuwa Mtwara Waliosekana Watu Wenye Sifa Hiyo Iliyohitajika.
Katika Suala Hili Wanafunzi 35 Wangweza Kusomeshwa Kwa Kulipiwa Ada Zaidi Ya Million Moja Lakini Pia Kwa Upande Mwingine Alielekeza Lawama Kwa Walimu Wa Masomo Kufanya Bidii Katika Masomo Yao Kwani Haiwezekani Mwalimu Unafundisha Mwaka Mzima Na Somo Lako Wanafunzi Wanapata Sufuri Hili Nalo Ni Tatizo La Elimu Kwa Huku Kusini Hususani Mtwara.

No comments:

Post a Comment