NA: MWANDISHI WETU
Wananchi wa mkoa wa Mtwara wametakiwa kuwa na utaratibu wa kutoa ushirikiano wa kutosha pindi fursa mbali mbali zinapojitokeza.
Rai hiyo imetolewa na shirika lisilo la kiserikali la compassion international
linaliojihusisha na huduma kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu, ambalo
limeanza kutoa huduma zake rasmi hivi leo katika maeneo ya raha leo opharnege
center mkoani Mtwara.
Akizungumza na wananchi mwezeshaji wa shirika hilo
Audats kisato, amesema kuwa wao kama compassion international wameamua
kuhudumia jamii ya watu wa mtwara, baada ya kufanya hivyo katika mikoa tofauti
nchini kwa lengo la kuikwamua jamii kutoka katika umaskini na hali ngumu ya
maisha.
Kisato amesema kuwa shirika hilo lenye makao makuu
nchini marekani katika jimbo la Colorado, limefanikiwa kufadhili watoto katika
nchi 28 ambazo kati ya hizo 12 ni nchi za afrika, ikiwemo Tanzania Kenya na Uganda.
Hata hivyo amewatoa wananchi wasiwasi kwa kueleza kuwa shirika hilo
limesajiliwa na kufahamika kisheria, na katika nchi ya Tanzania makao makuu
yake yako mkoani arusha, ambako ndiko
waliko anzisha huduma hizo mnamo april mwaka 1999.
No comments:
Post a Comment