EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Tuesday, February 18, 2014

NGAMLAGOSI ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MKUU WA EWURA

Felix NgamlagosiWAZIRI wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe,  amemteua Felix Ngamlagosi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), kuanzia Februari mosi mwaka huu.
Ngamlagosi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Haruna Masebu, aliyemaliza muda wake Desemba 31 mwaka jana  baada ya kuitumikia mamlaka hiyo kwa vipindi viwili vya miaka minne kila kimoja.
Taarifa kwa umma iliyotolewa jana na Mwenyekiti wa Ewura, Simon Sayore, ilieleza kabla ya uteuzi wake, Ngamlagosi alikuwa Mkurugenzi wa Udhibiti wa Kiuchumi wa Ewura, nafasi aliyoitumikia kwa miaka saba.

No comments:

Post a Comment