Imeandaliwa na Mshamu Ngojwike
NI wanakijiji haswa!
Walianza kama utani, kijiwe cha wazee wenye busara tu na ndio waanzilishi wa
timu. Si wengine ni Ndanda Fc, ambao wameleta gumzo kubwa kila kona mitaa ya Mkoa
wa Mtwara, ama kwa hakika wamewarudisha kwenye enzi za Bandari Fc.
Gumzo hilo si kwa mkoa
wa Mtwara tu, hata wapenzi wa kandanda
la hapa bongo walifuatilia toka kupanda kwao Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.
Ndipo ikaanza
minong'ono mingi huku wakihoji uwezo walio nao wakusakata kabumbu vijana hawa wameutowa wapi? Pamoja na sapota
kubwawanayoipata kutoka kwa mashabiki wa mikoa ya kusini mwa Tanzania ya Lindi na Mtwara.
Mashabiki hawa
walionyesha mbwenbwe haswa toka timu hiyo ikiwa ligi daraja la kwanza iwe
kwenye uwanja wa nyumbani ama nje ya Mtwara walikuwa wanatoa nguvu kubwa ya
kuisapoti.
Kwa wakifuata falsafa
ambazo wakitumia mashabiki wa Mbeya City msimu uliopita kwenye Ligi Kuu
Tanzania Bara,na muda ule wapo Ligi Daraja la Kwanza(FDL) nao.
Ndanda ilikuwa timu
ya kwanza kufanikiwa kupanda daraja msimu huu,baada kufanikiwa kuongoza kwenye
kundi A kwa pointi 28 ikiwa mbele kwa alama moja ya African Lyon iliyomaliza
ligi daraja la kwanza(FDL) kwa alama 27.
Lilikuwa kundi ambalo
lilitawaliwa timu za Mkoa wa Dar es Salaam ambazo zinatambua radha ya Ligi Kuu
zikiwemo African Lyon,Tessema,Friends Rangers na Polisi Dar.
Mbali na Ndanda Fc,
timu nyingine zilizopanda Ligi Kuu Mwaka huu ni pamoja na Stand United ya
Shinyanga na Polisi Morogoro kwa kuchukua nafasi ya Rhino Rangers, JKT Oljoro
na Ashanti United zilizoshuka daraja.
Zikiwa zimesalia siku
chache ili msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2014/2015 uanze kunguruma kwenye
viwanja tofauti hapa nchini, kila timu ipo katika maamdalizi ya kuanza msimu
mpya wa Ligi kwa kuweka kambi mikoa
tofauti tofauti ya hapa nchini.
Wageni hao, waliweka kambi
yao ya siku 40 jijini Dar es Salaam huku
wakichimbia kwenye Chuo Kikuu cha Ardhi wakijiwinda na Ligi hiyo inayotarajiwa
kuanza Septemba 20 mwaka huu.
Mtandao huu ulitinga kwenye
makao makuu ya klabu, kijijini kwao Ndanda Wilaya ya Masasi, Mkoani Mtwara. Na
kudaka historia ya ndanda Fc na Mikakati
yao kwenye Ligi mwaka huu, ambayo ilisimuliwa na mwenyekiti Ahamadi Omari Ally.
wanamtwara kuchele ndani ya ligi daraja la kwanza
HISTORI YAO
Mwenyekiti wa Ndanda Fc, Ahmadi Omari anasimulia
kuwa ilikuwa Machi 2011 yeye pamoja na
Jofrey Lukanga 'Jb' walipokutana na wakashaulina kunzisha timu maeneo ya Shule ya
Msingi Ndanda, ili kuleta upinzani na timu ya sokoni boda boda Fc, huku
ikifahamika kama Madukani Fc.
Ndipo mwezi huo huo
waliianzisha timu ya Ndanda Fc,wakiwa na lengo la kukuza vipaji kwa vijana wa kijiji cha Ndanda pamoja na kusini
kwa ujumla.
Aprili 2011, waliona
si busara kuwa na timu bila uongozi ndipo wakachagua benchi la viongozi ambao
waliongoza kikosi hicho chini ya mzee
Ahmadi Omari kama Mwenyekiti,Jofrey Lukanga mlezi wa timu kutokana yeye alikuwa
vizuri kiuchumi na John Mnunduma katibu.
Kwa muda huo kulikuwa
na upinzani mkubwa katika kijiji, baina ya timu ya Boda boda Fc,Sokoni Fc,wao
Ndanda Fc na timu ya Kiwanda cha maji ya Ndanda ambayo ikifadhiliwa na meneja
wa kampuni Mohamedi Mamu kutokana na kandanda safi ambalo walikuwa wanaonyesha
enzi hizo.
Lakini nyota ya Ndanda
Fc ilianza kung’aa toka mwaka huo huo wa 2011 baada ya kushiriki kombe la kugombea jezi na mipira
miwili ambalo liliandaliwa na Chama cha Soka Wilaya ya Masasi na kuafanikiwa kuibuka
mabingwa wa michuano hiyo.
Ndipo Mwishoni mwa
mwaka huo, timu hiyo ilishiriki ligi daraja la nne, na walifanikiwa kupanda
daraja hadi la tatu baada ya kuongoza kwa pointi kwenye mzunguko , ambapo
anasema muda huu timu ilikuwa chini ya kocha Samsoni Mrope ambaye kwa sasa ni
fundi gereji.
2012, walishiriki kwa
mara ya kwanza ligi daraja la ngazi ya Wilaya ya Masasi.Pia, hapa walifanikiwa
kupanda hadi ligi daraja la pili ngazi ya Mkoa wa Mtwara baada ya kuongoza kwa
alama kwenye hatua ya mzunguko na kuwa mwakilishi wa Wilaya ya Masasi.
Anasema 2012 hiyo
hiyo,walicheza ligi daraja la pili mwishoni mwa mwaka ili 2013 ipatikane timu
ambayo itawakilisha Mkoa wa Mtwara kwenye ligi daraja la kwanza(FDL) ngazi ya
taifa.Napo ilikuwa njia nyepesi kwao, maana walifanikiwa kupanda kwa mara ya
kwanza kushiriki ligi daraja la kwanza.
Walianza kushiriki
ligi daraja la kwanza 2013, ambapo hawakufanya vizuri walishika nafasi ya 3
kwenye kundi A, huku Ashanti United wakipanda msimu huo.
2014 ilikuwa mara yao
ya pili kushiriki ligi daraja la kwanza na kufanikiwa kupanda Ligi Kuu Tanzania
Bara msimu huu baada ya kusota kwa kipindi hicho cha miaka miwili, huku
zikizibwaga timu za mkoa wa Dar es Salaam.
CHIMBUKO LA JINA LA NDANDA FC:
Walitoa heshima ya
mto wa Ndanda ambao kwa wakazi wa kijiji hicho huutumia kwa shughuri zao za
kila siku pamoja na kilimo kando kando
yam to huo. Pia, Kampuni ya Maji ya Ndanda ‘Ndanda Springs Water’ hutumia maji
ya mto huu na kuyatengeneza kwa kuyachuja na kuyasambaza, ndipo wakaona
wautangaze mto huu kwa kutumia mpira na kuipa jina timu hii, jima la Ndanda Fc.
JINA UTANI
Kila timu za hapa
nyumbani hazikosi kuwa na jina la utani, kwa upande wa timu ya Ndanda wao
hufahamika kama ‘Walima Maji’. Baada ya timu hii kuanza kufadhiliwa na Kampuni
ya Maji ya Ndanda spring Water chini ya mkurugenzi wa kiwanda Mohamedi Mamu
pindi wakiwa Ligi Daraja la pili.
Muda huo maji
yalikuwa yakipatikana kwa wingi katika michezo yao, pamoja ya sifa ya mto
Ndanda ndipo wakawapachika jina la walima maji.
KAULI MBIU
Kama uliwahi
kushuhudi michezo yao muda wakishriki Ligi Daraja la Kwanza msimu uliopita basi
mashabiki wao, walikuwa wanastahili mpya
ya ushangiliaji ya kuiimba Ndandaa! Ndandaa! Kwa roho safi…! Na ndiyo
wamehitumia kuwa kauli mbiu yao kuwa ‘kwa roho safi’.
Wakimaanisha kuwa
ukiipenda timu yao basi utakuwa mtu wa furaha na uwe umeipenda toka kwenye
moyoni.
MWENYEKITI WA TIMU
Klabu hii inaongozwa
na mzee Ahmadi Omari Ally, ndiyo mwanzilishi wa timu,alianza kuongoza toka 2011 hadi inaipanda ligi Kuu ikiwa chini ya
uongozi wake.
KATIBU WA KLABU
Edmund Njoweka ndiyo
katibu Mkuu wa klabu. Alipata nafasi hii baada ya timu kuibadirisha kutoka
mikononi mwa wanachama hadi kuwa chini ya kurugenzi.
Ambapo ilibidi
wagawane wajumbe sita kutoka Mtwara mjini na sita toka Ndanda kijijini, ndipo
katibu huyu mkuu alipopta fursa ya kuongoza kuanzia mwaka huu.
NAHODHA
Baada ya kufanya
usajili wa nguvu, wakaamua kumpa nahodha mzawa toka nyumbani kwa Masasi Paul
Ngalema.
KOCHA
MKUU
Kocha Mkuu wa timu
hii Denis Kitambi,alichaguliwa baada ya kuchukua mikoba kutoka kwa Amri Saidi
ambaye aliibwaga ikiwa katika nafasi mbaya huku ikikabiliwa na michezo migumu
na kufanikisha kuipandisha daraja. Ndipo uongozi wa timu hii wakaona ni bora
waendelee naye.
UWANJA
Ndanda Fc watatumia
Uwanja wa Nangwanda Sijaona zamani ukijulikana kama Umoja. Mwaka huu, Uwanja
huu umefanyiwa ikarabati ili kuwa kwenye hadhi ya kutumika kwenye Ligi Kuu
Tanzania Bara.
MALENGO YAO
Anasema wamejipanga kuleta
ushindani kwenye Ligi Kuu mwaka huu, na wasidhani kama wamekuja kupanda pantoni
yaani kupanda na kushuka la hasha! Wamejidhatiti kuja kuonyesha maajabu ili
kuwa miongoni mwa timu vigogo hapa nchini.
USAJILI
Sehemu kubwa ya kikosi chao kitaundwa na vijana 14
ambao wameipandisha Klabu hiyo toka Ligi daraja la kwanza(FDL), huku wakifanya
usjili wa wachezaji 13 ambao ni wazoefu wa Ligi Kuu Tanzania Bara na kufika idadi
ya wanandinga 27 waliowasajili.
Wanaamini usajii
wachezaji walio ingia nao ni makini hivyo waweza kumudu mikiki mikiki ya Ligi
Kuu Tanzania Bara.
UDHAMINI
Miongoni mwa Klabu
imepata bahati ya mtende mwaka huu, ni pamoja na timu ya Ndanda. Hii ni kutokan
ni mara ya kwanza kushiriki ligi na wamepata wadhamini watatu nje na wadhamini
wa Kuu wa Ligi Vodacom na Azam tv.
Ndanda Fc, wanamaji
ya Ndanda Spring Water,Kampuni ya gesi ya BG Tanzania na Bin Slum ambao
wameingia udhamini kwenye klabu hiyo.
Kujiweka
Kibiashara
Amesema watauza vifaa
mbali mbali ambavyo waliagiza toka China katika mechi zao za Ligi Kuu Tanzania bara mwaka huu, lakini aliwataka
wapenzi wandanda Fc kutonunua vifaa feki
zenye nembo ya timu ya Ndanda kwani hadi sasa haijaanza kusambaza vifaa vya
aina yeyote nchini.
Vifaa hivi wameagiza
kutokana na soko lao la biashara na mahitaji husika ya eneo lao la kanda ya
kusini.Ambapo wameagiza jezi,kanga,kalenda na Stika vyema nembo ya timu ya
Ndanda Fc.
Sapoti
ya Mkoa
Chama Cha Soka Mkoa
wa Mtwara(MTWAREFA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ipo bega
kwa bega kwa kuwatafutia wadhamini kama BG Tanzania ni nguvu ya Mkuu Mkoa wa
Mtwara Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia.
Walitumia harambee ya
kuwakutanisha viongozi mbali mbali kwenye kampeni ya Changia Ndanda Ishinde
wakati ipo kwenye mchakato wa kutafuta nafasi nya kupanda ligi kuu msimu huu.
Jina la timu:Ndanda Fc
Jina la Utani:Walima maji
Ilianzishwa:2011
Mwenyekiti:Ahmadi Omari Ally
Katibu:Edmund Njoweka
Kocha Mkuu:Denis Kitambi
Nahodha:Paul Ngalema
Uwanja:Nangwanda Sijaona
No comments:
Post a Comment