EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Thursday, March 6, 2014

MAMA MZAZI WA KANUMBA KUOZEA JELA KISA MALI ZA MWANAE STEVEN KANUMBA


BABA wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba anaonekana kuendelea kuwewesekea mali za mwanaye baada ya kuibuka na kudai kuwa, atampeleka Segerea (jela) mzazi mwenzake, Flora Mtegoa kwa madai kuwa amezifuja mali za marehemu.
Mama Kanumba, Flora Mtegoa.
Akizungumza na SWACOTZ FORUM hivi karibuni kwa njia ya simu, baba Kanumba alisema, ameona taarifa kwenye gazeti kuwa mali nyingi za marehemu Kanumba zimeuzwa huku yeye akiwa hajaambulia chochote.
“Huyu mama Kanumba ana laana yangu, amefuja mali za mwanangu kwa kushirikiana na Seth, mimi sijashirikishwa, nisipopata chochote tutafikishana pabaya,” alisema mzee huyo.
Baba wa marehemu Kanumba, Charles Kanumba.
Kuhusiana na hilo, mama Kanumba huyu hapa: “Kwa mila za Kisukuma Kanumba siyo mwanaye kwa kuwa hajanioa, hivyo kuhusu suala la mali kama anazijua zinazomhusu aonyeshe moja baada ya nyingine hapo itakuwa sawa.”

No comments:

Post a Comment