EBENEZA MARCH 9 2014

EBENEZA MARCH 9 2014

Friday, January 17, 2014

MVUA MTWARA YAKOSESHA KAYA 37 MAKAZI



NA: KASSIM NGUMBI
Kaya Thelathin Na Saba Za Vijiji Vine Vya Kata Ya Nanyamba Katika Halmashauri Ya Mji Mdogo Wa Nanyamba Zimejikuta Zikiingia Katika Hali Ya Sintofaham Na Baadhi Kukosa Mahali Pa Kuishi Baada Ya Nyumba Walizokuwa Wakiishi Kubomolewa Na Mvua Iliyoambatana Na Upepo Mkali Ambayo Imenyesha Usiku Wa Kuamkia Leo.
Akizungumza Katika Ofisi Ya Kata Ya Nanyamba Mbele Ya Wahanga Wa Tukio Hilo Mkuu Wa Wilaya Ya Mtwara Mh: Wilman Kapenjama Ndile Aliyekuwa Ameambatana Na Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri Ya Wilaya Mtwara Vijijini Katika Ziara Ya Kuwapa Pole Wahanga Hao Alisema Kuwa Serikali Imepokea Kwa Masikitiko Makubwa Taarifa Za Tukio Hilo Zilizotolewa Na Diwani Wa Kata Hiyo  (Ccm) Mh: Mmauji  Na Ndioyo Maana Imefika Kuwatembelea.
Aidha Mkuu Huyo Wa Wilaya Aliwataka Wananchi Kuwa Na Subra Katika Kipindi
Hiki Na Wale Ambao Numba Zao Zimeharibika Kabisa Basi Wajishikize Kwa Ndugu Na Jiran  Huku Serikali Ikiangalia Namna Ya Kuwasaidia Ingawa Hakusema Iwapo Watu Hao Wangesaidiwa Gharama Za Ujenzi Licha Ya Kuahidi Kuwapatia Msaada Wa Chakula Ifikapo Jumanne Ijayo Ya Tarehe 21 Mwezi Huu.

Katika Safari Yake Mkuu Wa Wilaya Alitembelea Maeneo Yaliyotokea Matukio Hayo Na Kujionea  Maafa Makubwa Yaliyoachwa Na Mvua Hizo Ikiwamo Kubomolewa Kwa Makazi Ya Watu Pamoja Na Uharibifu Wa Mimea Ya Mazao Kama Vile Mikorosho.
Hata Hivyo Hakuna Mtu Aliyeripotiwa Kujeruhiwa Wala Kufariki Dunia Mpaka Sasa Kutokana Na Tukio Hilo Hali Inayopelekea Wakazi Wa Eneo Hilo Kumshukuru Mungu Kwakuwa Wote Wameweza Kunusuruika  Kwa Upande Wake Diwani Wa Kata Hiyo Mh, Mmauji Alieleza Tukio Hilo Kuwa  Si Lakawaida Kwani Haijawahi Tokea Kwa Kipindi Cha Hivi Karibuni Huku Akimshukuru Mkuu Wa Wilaya Na Mkurugenzi Kwa Kuja Haraka Kujionea Na Kuwapa Pole Wananchi Hali Ambayo Itarejesha Matumaini Kwa Wananchi Hao.

No comments:

Post a Comment