WANAFUNZI wa Manispaa ya Mtwara Mikindani wametoa
maoni yao, juu ya matumizi ya maktaba ya mkoa, iliyopo maeneo ya maduka makubwa
mjini Mtwara, na kuomba utaratibu wa kuingia na kutoka katika maktaba hiyo
uwekwe bayana.
Wakizungumza na mwandishi wa Pride Fm Redio katika
eneo la maktaba
hiyo, mmoja wa wanafunzi hao kutoka shule ya sekondari ya Chuno
Mohamed Mussa amesema kuwa, ni vyema maktaba ikatoa utaratibu wa wananfunzi wa
kuingia katika maktaba hiyo, kutokana na maktaba ya shule yao kutokidhi
mahitaji ya wanafunzi hao.
Aidha Mohamedi ameongeza kuwa na ni vyema kwa uongozi
wa shule ya Sekondari ya Chuno ukafutilia utaratibu wa maktaba hiyo ya Mkoa, ili
kuwapa wanafunzi utaratibu utakaokuwa pale na hiyo itawapatia nafasi za kujifunza
zaidi.
Mwanafuzi mwingine kutoka shule ya sekondari
Shangani Walivyo Fadhil, amesema kuwa ni vyema kwa maktaba ya Mkoa ikatoa fursa
za eneo hilo la utaratibu, kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kutanua wigo wa
wanafunzi wa shule zote zilizopo katika mkoa wa Mtwara kujisomea.
ENDELEA ZAIDI
No comments:
Post a Comment