Dunia ina mengi....Dawa ya tatizo ni kukubaliana nalo.
Huyu ni jamaa mwenye jinsia mbili na kwa mujibu wa maelezo
yake anadai kuwa jinsia zote mbili ziko poa (Active)..
Kinachofurahisha zaidi ni kwamba jamaa kakubaliana na
tatizo...Haoni kama ni shida na anaisha maisha ya kawaida
kabisa...
Cha kufurahisha zaidi ni kwamba, jamaa katangaza kusaka
mchumba ...
FEZA KESSY AENDELEA KUPETA NDANI YA BIG BROTHER.....MPENZI WAKE ATOLEWA
Hatimaye jina la Oneza limefikia tamati jana baada ya Afrika kuamua
kumuondoa shemeji yetu Oneal aliyepata kura ndogo zaidi katika The
Chase.
Pamoja na matumaini madogo sana aliyokuwanayo Feza ya kupona panga la
eviction ya jana (August 4) lakini Afrika imeamua kummbakiza Feza
mshiriki pekee wa Afrika mashariki na Tanzania aliyebaki.
Feza Kessy
amepona katika eviction ya jana kwa kura tatu tu za Tanzania, Kenya na
Sierra Leone , wakati Uganda wakiwa kama nchi ya Afrika mashariki
wameonekana kuchoshwa na mapenzi ya Oneza hivyo kura yao wakampa Bimp.
Bimp ndiye mshiriki aliyekuwa star wa eviction show ya jana sababu
ndiye...
ROBERT MUGABE NDANI YA IKULU YA ZIMBABWE KWA MARA YA SABA....
Baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kinyan’ganyiro cha Urais wa
Zimbabwe, Rais Robert Mugabe (89), amefikisha mihula saba ndani ya
Ikulu ya nchi hiyo.
Mugabe juzi alishinda tena kiti cha urais. Matokeo
rasmi yalionyesha kuwa aliibuka na ushindi wa asilimia 61 wa kura dhidi
ya mpinzani wake, aliyekuwa Waziri Mkuu, Morgan Tsvangirai ambaye
alipata asilimia 34.
Chama cha Zanu-PF kinachoongozwa na Mugabe na kile cha MDC cha Tsvangirai, viliunda Serikali ya Muungano mwaka 2008.
Juzi, Tume ya Uchaguzi Zimbabwe (ZEC), ilimtangaza Mugabe...
" NILIKURUPUKA KUOLEWA MAPEMA" JACK PATRICK
MWANAMITINDO marufu Bongo, Jacqueline Patrick ‘Jack’ amesema alikurupuka
kuolewa na aliyekuwa mume wake, Abdulatif Fundikira ‘Tiff’ kwa kuwa
hakufanya tathmini ya kina kabla ya kufanya maamuzi.
Akizungumza na mwandishi wetu, Jack alisema laiti angekaa kwenye uchumba
kwa angalau muda wa miaka miwili kuchunguzana kabla ya kuoana mwaka
2011, asingeweza kufikia hatua ya ndoa kwani wangeshindwana tabia
mapema.
“Nilikosea, nikakurupuka kuolewa mapema bila kumchunguza
tabia mpenzi wangu, uhusiano wetu ulidumu miezi mitano tu kisha
tukafunga ndoa, lakini matokeo yake tabia hazikuendana na ndoa ikakosa
uhai ndani ya muda...
No comments:
Post a Comment